Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Soma Biblia Kila Siku 6Mfano

Soma Biblia Kila Siku 6

SIKU 3 YA 30

Ikawa huko Ikonio wakingia pamoja katika sinagogi la Wayahudi; na kwa vile walivyonena, kundi kubwa la Wayahudi na la Wayunani wakaamini (m.1). Maelezo: 1. Wayahudi hawakukaa katika nchi ya Israeli tu bali walikuwa wameenea katika nchi zote na miji yote mikubwa. 2. Kila mahali walipokaa walikuwa wamejenga sinagogi. Kazi yake ilikuwa kama jengo la kanisa kwetu. 3.Utaratibu wa Paulo kila mahali alipofika ni kwanza kuingia katika sinagogi ili kuhubiri Injili, maana Injili ni kwa Wayahudi kwanza: Injili ... ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia(Rum 1:16).4. "Wayuani" ni Mataifa.

siku 2siku 4

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 6

Soma Biblia Kila Siku 6 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.

Tungependa kushukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha