Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Soma Biblia Kila Siku 6Mfano

Soma Biblia Kila Siku 6

SIKU 30 YA 30

Tafakari maneno haya pamoja na Sefania 2:3, Mtafuteni Bwana, enyi nyote mlio wanyenyekevu wa dunia, ninyi mliozitenda hukumu zake; itafuteni haki, utafuteni unyenyekevu; huenda mtafichwa katika siku ya hasira ya Bwana. Tunaitwa kumtafuta Mungu kila siku ya maisha yetu kwa kutega sikio letu kusikia neno lake ili atushikie hatua za mienendo yetu. Tukiweka bidii katika jambo hili, Mungu atatufinyanga upya tupate kipawa cha kumcha na kutushikamanisha naye. Ufahamu ulio bora ni ule unaomwelekea Mungu. Kwa hiyo wito wa leo ni kuweka bidii katika kumtafuta Mungu. Fanya hivyo kwa kuomba na kujifunza Neno lake kwa bidii. Hivyo utaongezeka maarifa ya kumwishi Mungu!

siku 29

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 6

Soma Biblia Kila Siku 6 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.

Tungependa kushukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha