Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Soma Biblia Kila Siku Mei/2022Mfano

Soma Biblia Kila Siku Mei/2022

SIKU 7 YA 31

Ufalme wa Sulemani ulipokuwa ukiimarika, Adonia alionyesha bado kutokuridhika. Alionyesha malalamikoakasema, Wajua ya kwamba ufalme ulikuwa wangu, na Israeli wote wakaniwekea nyuso zao ili nimiliki mimi; walakini sasa ufalme umegeuka kuwa wake ndugu yangu; kwa maana ulikuwa wake kutoka kwa Bwana(m.15). Tamaa yake ya kuwa mtu wa hadhi ilimsukuma Adonia kutaka aozeshwe Abishagi, binti aliyemtumikia mfalme Daudi. Kwa hila alimtaka Bath-sheba amwakilishe kwa mfalme Sulemani. Jambo hili lilimkasirisha mfalme. Aliona ni uhaini. Aliona Adonia akipewa anachoomba, Yoabu jemadari wa jeshi, na Abiathari kuhani watataka warudishiwe hadhi zao. Jambo hilo lilimletea Adonia kifo. Tamaa ni mbaya.

siku 6siku 8

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku Mei/2022

Soma Biblia Kila Siku Mei/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Mei pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma kwa sik...

More

Tungependa kuwashukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz/

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha