Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Soma Biblia Kila Siku 06/2020Mfano

Soma Biblia Kila Siku 06/2020

SIKU 1 YA 30

Mtume Yohana aliwaandikia Wakristo barua hii wakiwa kama watoto wake katika Mungu (m.18: Watoto, ni wakati …). Mpinga Kristo (m.18) ni mtu anayejiweka katika nafasi ya Kristo. Hujitegemea bila Mungu na bila Mwokozi. Walitoka kwetu (m.19). Wapinga Kristo hawatokei nje ya kanisa, bali wanatokea miongoni mwa washarika. Ni muhimu kuwatambua na kuwapiga vita! Wao ni dalili kwamba siku ya mwisho inakaribia. Pia inaonyesha kwamba tunaweza kuwa washarika bila kweli kumjua Kristo. Katikati ya kundi la Wakristo upo mpakausioonekana kwa macho unaowagawanya waumini na wasioamini katika vikundi viwili. Je, wewe na mimi tuko wapi?

siku 2

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 06/2020

Soma Biblia Kila Siku 06/20 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha 1 Yohana, Ayubu na Mathayo. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Kari...

More

Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha