Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Chuma Hunoa Chuma: Life-to-Life® Mentoring in the Old TestamentMfano

Iron Sharpens Iron: Life-to-Life® Mentoring in the Old Testament

SIKU 4 YA 5

Siku 4: Daudi na Yonathani



Urafiki wa pamoja kati ya Daudi na Yonathani unatoa picha nyingine ya kile mafunzo ya maisha na maisha yanavyoonekana. 



Mfalme Sauli alikuwa ni mfalme wa kwanza wa Israeli, na Yonathani alikuwa mwanaye. Ingawa alianza katika hali ya chini, Sauli pole pole alianza kutomheshimu Mungu na kuendelea kujenga ufalme wake. Sehemu ya ufalme huo unajitahidi kuhakikisha kwamba siku moja Yonathani angembadili kama mfalme.



Bado huo haukuwa mpango wa Mungu. Bali, Mungu alimuongoza nabii, Samweli, kumpaka mafuta kijana mdogo mchungaji Daudi kama mbadala wa Sauli. Daudi alikuwa " mpenzi wa Mungu." Bahati mbaya, mfalme Sauli alikuwa si kitu. Kwa hiyo, kutokana na wivu, Sauli bila kukoma alimuwinda Daudi ili amuue na kutoa njia kwa Yonathani kuchukua kiti cha enzi na kumbadili kama mfalme. (Angalia 1 Samueli 1-31.) 



Katikati ya vurugu zote hizi, kitu kisichotarajiwa kilitokea: Daudi na Yonathani wakawa marafiki; "moyo wa Yonathani ulishonana na moyo wa Daudi, na Yonathani alimpenda kama roho yake mwenyewe." Hakukuwa na mashindano, wala mashaka kwamba mmoja angeweza kuharibu uhusiano; wote wawili walijitoa kusaidiana kwa gharama yoyote.



Tunaona wito wa ushirika wa faida kwa pande zote mbili katika Biblia yote. Unaonekana katika mithali mbili hasa hasa: "Ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe; Lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu.” na “Chuma hunoa chuma; Ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki yake.” (Mithali 18:24; 27:17). 



Kutokana na urafiki wa Daudi na Yonathani, tunajifunza umuhimu wa mtu ambaye hakika "anakutetea." Hakika, kama mtoto wa Daudi Sulemani alivyoandika, afadhali kuwa wawili kuliko mmoja (Mhubiri 4:9-12), na Mungu katika uhusiano," na "wala kamba ya nyuzi tatu haikatiki upesi ” (v. 12). 


siku 3siku 5

Kuhusu Mpango huu

Iron Sharpens Iron: Life-to-Life® Mentoring in the Old Testament

Unatamani "kufanya wanafunzi wanaofanya wanafunzi," kufuatana na Yesu katika Agizo Kuu (Mathayo 28:18-20)? Kama ndivyo, yawezekana umeona kwamba inaweza kuwa vigumu kupata watu wa mfano katika mchakato huu. Utafuata mfan...

More

Tunapenda kuwashukuru The Navigators kwa kutupa mpango huu. Kwa taarifa zaidi, tafadhali tembelea: https://www.navigators.org/youversion

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha