YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 81

81
Wimbo wa sikukuu
(Kwa Mwimbishaji: Mtindo wa Gitithi. Zaburi ya Asafu)
1Mwimbieni kwa sauti Mungu, nguvu yetu,
mshangilieni Mungu wa Yakobo;
2vumisheni wimbo wa shangwe, pigeni ngoma,
chezeni zeze na kinubi cha sauti nzuri.
3Pigeni tarumbeta kutangaza mwezi mwandamo,
na pia mwezi mpevu, wakati wa sikukuu yetu.
4Hiyo ndiyo kanuni katika Israeli;
hilo ndilo agizo la Mungu wa Yakobo.
5Aliwapa watu wa Israeli agizo hilo,
alipoishambulia nchi ya Misri.
Nasikia sauti nisiyoitambua ikisema:
6“Mimi nilikutua mizigo yako mabegani,
nilikuondolea matofali uliyochukua mikononi.
7Ukiwa shidani uliniita, nami nikakuokoa.
Nilikujibu nikiwa mafichoni katika ngurumo.
Nilikujaribu kwenye maji ya Meriba.
8Enyi watu wangu, sikieni onyo langu.
Laiti ungenisikiliza, ee Israeli!
9Asiwepo kwako mungu wa kigeni;
usiabudu kamwe mungu mwingine.
10Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako,
niliyekutoa katika nchi ya Misri.
Fumbua kinywa chako, nami nitakulisha.
11“Lakini watu wangu hawakunisikiliza;
Israeli hakunitaka kabisa.
12Hivyo, nikawaacha wabaki na ukaidi wao;
wafuate mashauri yao wenyewe.
13Laiti watu wangu wangenisikiliza!
Laiti Israeli angefuata njia yangu!
14Ningewashinda maadui zao haraka;
ningenyosha mkono dhidi ya wadhalimu wao.
15Wanichukiao wangenipigia magoti kwa hofu,
na adhabu yao ingekuwa ya milele.
16Lakini wewe ningekulisha kwa ngano bora,
ningekushibisha kwa asali ya mwambani.”

Currently Selected:

Zaburi 81: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy