YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 82

82
Mungu mtawala mkuu
(Zaburi ya Asafu)
1Mungu anasimamia baraza lake;
anatoa hukumu katika kusanyiko la miungu:
2“Mpaka lini mtaendelea kuhukumu bila haki
na kuwapendelea watu waovu?
3Wapeni wanyonge na yatima haki zao;
tekelezeni haki za wanaoonewa na fukara.
4Waokoeni wanyonge na maskini,
waokoeni makuchani mwa wadhalimu.
5“Lakini nyinyi hamjui wala hamfahamu!
Nyinyi mnatembea katika giza la upotovu!
Misingi yote ya haki duniani imetikiswa!
6Mimi nilisema kuwa nyinyi ni miungu;
kwamba nyote ni watoto wa Mungu Mkuu!
7Hata hivyo, mtakufa kama watu wote;
mtaanguka kama mkuu yeyote.”
8Inuka ee Mungu, uuhukumu ulimwengu;
maana mataifa yote ni mali yako.

Currently Selected:

Zaburi 82: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy