YouVersion Logo
Search Icon

Yobu 36

36
1Kisha Elihu akaendelea kusema:
2“Nivumilie kidogo, nami nitakuonesha kitu;
maana bado ninacho cha kusema kwa niaba ya Mungu.
3Nitaleta hekima yangu kutoka mbali sana,
na kuonesha kwamba Muumba wangu ni mwadilifu.
4Kweli maneno yangu si ya uongo;
mwenye elimu kamili yuko hapa nawe.
5“Sikiliza Mungu ni mwenye nguvu
wala hamdharau mtu yeyote;
uwezo wa akili yake ni mkuu mno!
6Hawaachi waovu waendelee kuishi;
lakini huwapatia wanaodhulumiwa haki zao.
7Haachi kuwalinda watu waadilifu;
huwatawaza, wakatawala na kutukuka.
8Lakini kama watu wamefungwa minyororo,
wamenaswa katika kamba za mateso,
9Mungu huwaonesha matendo yao maovu,
na kwamba wao ni watu wenye kiburi.
10Huwafungua masikio wasikie mafunzo,
na kuwaamuru warudi na kuacha uovu.
11Wakimtii Mungu na kumtumikia,
hufanikiwa katika siku zao zote;
miaka yao yote huwa ya furaha.
12Lakini wasipomtii, huangamia kwa upanga,
na kufa kwa kukosa akili.
13“Wasiomcha Mungu hupenda kukasirika,
hawamlilii msaada anapowabana.
14Hufa wangali bado vijana,
maisha yao huisha kama ya walawiti.
15Lakini Mungu huwaokoa wanyonge kwa unyonge wao
hutumia shida zao kuwafumbua macho.
16Mungu alikuvuta akakutoa taabuni,
akakuweka mahali pa wasaa pasipo shida,
na mezani pako akakuandalia vinono.
17“Lakini sasa umehukumiwa kama mwovu,
hukumu ya haki imekukumba.
18Jihadhari ghadhabu isije ikakufanya ukadhihaki,
au ukubwa wa mali za kukukomboa ukakupotosha.
19Je, kilio chako kitafaa kukutoa taabuni,
au nguvu zako zote zitakusaidia?
20Usitamani usiku uje,
ambapo watu hufanywa watoweke walipo.
21Jihadhari! Usiuelekee uovu
maana umepatiwa mateso kukuepusha na uovu.
22Kumbuka ukuu wa uwezo wa Mungu;
nani awezaye kumfundisha kitu?
23Nani basi aliyeweza kumpangia njia yake,
au awezaye kumwambia: ‘Umekosea?’
24“Usisahau kuyasifu matendo yake;
ambayo watu wameyashangilia.
25Watu wote wameona aliyofanya Mungu;
binadamu huyaona kutoka mbali.
26Mungu ni mkuu mno hata hatuwezi kumjua;
muda wa maisha yake hauchunguziki.
27Yeye huyavuta kwake maji ya bahari,
na kutoka ukungu hufanya matone ya mvua.
28Huyafanya mawingu yanyeshe mvua,
na kuwatiririshia binadamu kwa wingi.
29Nani ajuaye jinsi mawingu yatandavyo,
au jinsi radi ingurumavyo angani kwake?
30Yeye huutandaza umeme wake kumzunguka,
na kuvifunika vilindi vya bahari.
31Kwa mvua huwalisha#36:31 huwalisha: Au huwahukumu. watu
na kuwapatia chakula kwa wingi.
32Huukamata umeme kwa mikono yake,
kisha hulenga nao shabaha,
33Radi hutangaza ujio wake Mungu,
hata wanyama hujua kwamba anakuja.

Currently Selected:

Yobu 36: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy