YouVersion Logo
Search Icon

Yobu 35

35
1Kisha Elihu akaendelea kusema:
2“Je, Yobu, unaona jambo hili ni sawa
na kufikiri kinyume cha Mungu
3ukiuliza: ‘Nimepata faida gani
kama sikutenda dhambi?
Nimefaidika kuliko kama ningalitenda dhambi?’
4Mimi nitakujibu wewe,
na rafiki zako pia.
5Hebu zitazame mbingu!
Tazama mawingu yaliyo juu kuliko wewe!
6 # Taz Yobu 22:2-3 Ukitenda dhambi, je, Mungu ndiye unayemdhuru?
Na kama ukizidisha makosa yako, wadhani unamwumiza?
7Kama wewe ni mwema, je, unampatia faida,
au yeye anapokea kitu kutoka kwako?
8Uovu wako utamdhuru binadamu kama wewe,
wema wako utamfaa binadamu mwenzako.
9“Kwa sababu ya udhalimu mwingi watu hulia,
huomba msaada kwa sababu ya mapigo ya wenye nguvu.
10Lakini hakuna asemaye, ‘Yuko wapi Mungu, Muumba wangu,
mwenye kunifanya niwe mchangamfu usiku,
11anayetuelimisha kuliko wanyama,
na kutufanya wenye hekima kuliko ndege!’
12Watu hao huomba msaada lakini Mungu hawajibu,
kwa sababu ya majivuno ya watu waovu.
13Kweli Mungu hasikilizi kilio cha bure;
Mungu Mwenye Nguvu hajali kilio hicho.
14Atakujibu vipi wakati wewe
unasema kwamba humwoni
na kwamba kesi yako iko mbele yake
na wewe unamngojea!
15Sasa, kwa vile Mungu anazuia hasira yake,
wala hajali sana makosa ya watu,
16Yobu unafungua mdomo kusema maneno matupu,
unazidisha maneno bila akili.”

Currently Selected:

Yobu 35: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy