YouVersion Logo
Search Icon

Hosea 6

6
Toba isiyo ya kweli
1“ ‘Twendeni, tukamrudie Mwenyezi-Mungu!
Yeye mwenyewe ameturarua,
lakini yeye mwenyewe atatuponya.
Yeye mwenyewe ametujeruhi,
lakini yeye mwenyewe atatibu majeraha yetu.
2Baada ya siku mbili, atatupa uhai tena,
naam, siku ya tatu atatufufua
ili tuweze kuishi pamoja naye.
3Basi tumtambue,
tujitahidi kumjua Mwenyezi-Mungu.
Kuja kwake ni hakika kama alfajiri,
yeye atatujia kama manyunyu,
kama mvua za masika ziinyweshayo ardhi.’”
4Lakini Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Nitakutendea nini ee Efraimu?
Nikufanyie nini ee Yuda?
Upendo wenu kwangu ni kama ukungu wa asubuhi,
kama umande unaotoweka upesi.
5Ndiyo maana nimewavamia kwa njia ya manabii,
nimewaangamiza kwa maneno yangu,
hukumu yangu huchomoza kama pambazuko.
6Maana ninachotaka kwenu ni upendo na si tambiko,
Kumjua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa.
Uhalifu umeenea kote nchini
7“Lakini mlilivunja agano langu
kama mlivyofanya mjini Adamu;
huko walinikosea uaminifu.
8Gileadi ni mji wa waovu,
umetapakaa damu.
9Kama wanyang'anyi wamwoteavyo mtu njiani,
ndivyo na makuhani walivyojikusanya na kuvizia.
Wanaua watu njiani kuelekea Shekemu,
naam, wanatenda uovu kupindukia.
10Nimeona jambo la kuchukiza sana
miongoni mwa Waisraeli:
Watu wa Efraimu wanakimbilia miungu mingine
naam, Waisraeli wamejitia unajisi.
11Nawe Yuda hali kadhalika,
nimekupangia wakati utakapovuna adhabu.

Currently Selected:

Hosea 6: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy