Maelezo ya mpango
Soma Biblia Kila Siku Oktoba/2022Mfano
Je, tuombe uponyaji kwa Yesu kwa namna gani? Jambo la msingi ni unyenyekevu ambao huyu mgonjwa alimwonyesha Yesu kwa njia mbili: 1. Alipomwona Yesu alianguka kifudifudi 2. Akamwomba akisema, Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa (m.12). Unyenyekevu huu unatakiwa maana hatustahili kusaidiwa naye, hatuna haki kudai uponyaji. Tunayostahili ni kupigwa na hasira yake. Kwa hiyo tunayohitaji ni kwamba atuhurumie kwa neema yake. Pia hatujui mapenzi yake, labda muda wetu wa kuondoka duniani umefika. Tafakari ombi hili “ukitaka”, ukililinganisha na ombi la Baba yetu: Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni (Mt 6:10).
Andiko
Kuhusu Mpango huu
Soma Biblia Kila Siku Oktoba/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Oktoba pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu ulilosoma k...
More
http://www.somabiblia.or.tz