Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Soma Biblia Kila Siku Februari/ 2022Mfano

Soma Biblia Kila Siku Februari/ 2022

SIKU 3 YA 28

Kristo alitiwa mhuri kama Masiha na Mungu Baba (Yn 6:27,Mwana wa Adamu ... huyo ndiye aliyetiwa muhuri na Baba, yaani, Mungu). Kwenye msingi huu, waumini waliookolewa na Kristo wametiwa mhuri na Roho Mtakatifu (m.13,Nanyi pia katika huyo mmekwisha ... kutiwa muhuri na Roho yule wa ahadi aliye Mtakatifu). Wakati wa Paulo mhuri ulionyesha umiliki. Waumini ni mali ya Mungu. Mungu ametutia mhuri kwa kutupatia Roho wake ndani ya mioyo yetu kama dhamana (2 Kor 1:22,Naye ndiye aliyetutia muhuri akatupa arabuni ya Roho mioyoni mwetu). Kama alama, kutiwa mhuri huu unamaanisha umiliki wa muumini na Mungu, na uhakika wa wokovu na urithi ule atakaoupokea siku ya ukombozi kamili (4:30,Yule Roho Mtakatifu wa Mungu ... kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi). Je, wewe umeshatiwa mhuri huu?

siku 2siku 4

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku Februari/ 2022

Soma Biblia Kila Siku Februari/2022 ni mpango wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku kwa mwezi wa Februari pamoja na maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa kwa urahisi na kuendelea kutafakari neno la Mungu uliloso...

More

Tungependa kushukuru Soma Bible kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz/

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha