Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Soma Biblia Kila Siku Mei 2021Mfano

Soma Biblia Kila Siku Mei 2021

SIKU 8 YA 31

Yesu akawauliza, Ni halali siku ya sabato kutenda mema, au kutenda mabaya? kuponya roho au kuiua? Wakanyamaza (m.4). Sabato kwa Wayahudi ni kama Jumapili ilivyo kwetu, yaani, siku ya kumwabudu Mungu na siku ya kupumzika. Kama Mwana wa Mungu, Yesu alijua maana ya sabato kuliko mtu mwingine. Ndiye Bwana wa sabato (2:28). Na kuhusu uhusiano wa sabato na mwanadamu, mafundisho yake ni wazi: Sabato ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu, si mwanadamu kwa ajili ya sabato (2:27)! Lakini Mafarisayo walifungwa na mapokeo ya wazee hata wasiweze kulifurahia tendo jema (ling. m.5-6 tunaposoma: Yesu akawakazia macho pande zote kwa hasira, akiona huzuni kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao [hapo waliponyamaza Yesu alipowauliza kama ni halali kutenda mema siku ya sabato], akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Naye akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena. Mara wakatoka wale Mafarisayo, wakawa wakifanya shauri juu yake pamoja na Maherodi, jinsi ya kumwangamiza.

Andiko

siku 7siku 9

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku Mei 2021

Soma Biblia Kila Siku Mei 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Marko na Ayubu. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu kujiun...

More

Tungependa Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha