Maelezo ya mpango
Soma Biblia Kila Siku 7Mfano
Paulo alizidi kuwapenda wasafiri wenzake. Bila shaka alikuwa amewaombea sana kwa Mungu. Na Mungu aliwapa neno la tumaini kwa kupitia mtumishi wake Paulo (m.21-26). Sasa wakamsikiliza sana Paulo (taz. m.35-36:Alipokwisha kusema hayo akatwaa mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote akaumega akaanza kula. Ndipo wakachangamka wote, wakala chakula wenyewe) na ikatokea kama alivyokuwa ametabiri. Wote wakasalimika (m.44b:Watu wote wakapata kuifikilia nchi kavu salama). Kuna maneno yanayoeleweka zaidi kwa tafsiri ya Biblia Habari Njema: “tukadiriki” (m.16) = tuliwahi kuokoa kabla hayajaharibika.“fungu liitwalo Sirti” (m.17) = ufuko wa bahari, pwani ya Libya. “hori yenye ufuo” (m.39) = ghuba moja yenye ufuko.
Andiko
Kuhusu Mpango huu
Soma Biblia Kila Siku 7 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku pamoja na maelezo yatakayokusaidia kuelewa zaidi.
Tungependa kushukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz