Methali 2:8-13
Methali 2:8-13 Biblia Habari Njema (BHN)
Huilinda mienendo ya watu watendao haki, na kuzihifadhi njia za waaminifu wake. Ukinisikiliza utafahamu uadilifu na haki, utajua jambo lililo sawa na jema. Maana hekima itaingia moyoni mwako, na maarifa yataipendeza nafsi yako. Busara itakulinda, ufahamu utakuhifadhi; vitakuepusha na njia ya uovu, na watu wa maneno mapotovu; watu waziachao njia nyofu, ili kuziendea njia za giza
Methali 2:8-13 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Apate kuyalinda mapito ya hukumu, Na kuhifadhi njia ya watakatifu wake. Ndipo utakapofahamu haki na hukumu, Na adili, na kila njia njema. Maana hekima itaingia moyoni mwako, Na maarifa yatakupendeza nafsi yako; Busara itakulinda; Ufahamu utakuhifadhi. Ili kukuokoa na njia ya uovu, Na watu wanenao yaliyopotoka; Watu waziachao njia za unyofu, Ili kuziendea njia za giza
Methali 2:8-13 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Apate kuyalinda mapito ya hukumu, Na kuhifadhi njia ya watakatifu wake. Ndipo utakapofahamu haki na hukumu, Na adili, na kila njia njema. Maana hekima itaingia moyoni mwako, Na maarifa yatakupendeza nafsi yako; Busara itakulinda; Ufahamu utakuhifadhi. Ili kukuokoa na njia ya uovu, Na watu wanenao yaliyopotoka; Watu waziachao njia za unyofu, Ili kuziendea njia za giza
Methali 2:8-13 Neno: Bibilia Takatifu (NEN)
kwa kuwa hulinda mwenendo wa mwenye haki na kuhifadhi njia ya waaminifu wake. Ndipo utafahamu lipi lililo kweli na haki na sawa: yaani kila njia nzuri. Kwa maana hekima itaingia moyoni mwako, nayo maarifa yataifurahisha nafsi yako. Busara itakuhifadhi na ufahamu utakulinda. Hekima itakuokoa kutoka njia za waovu, kutoka kwa watu ambao maneno yao yamepotoka, wale waachao mapito yaliyonyooka wakatembea katika njia za giza