Kumbukumbu la Sheria 30:15-16
Kumbukumbu la Sheria 30:15-16 Biblia Habari Njema (BHN)
“Leo hii nawapeni uchaguzi kati ya mema na mabaya; kati ya uhai na kifo. Kama mkitii amri za Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, ambazo ninawapa leo, mkampenda Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, na kufuata njia zake na kushika masharti na maagizo yake, basi, mtaishi na kuongezeka; naye Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, atawabariki katika nchi ambayo mnakwenda kuimiliki.
Kumbukumbu la Sheria 30:15-16 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya; kwa hivi nikuagizavyo leo kumpenda BWANA, Mungu wako, kuenenda katika njia zake, na kushika maagizo yake, na amri zake, na hukumu zake, upate kuwa hai na kuongezeka; BWANA, Mungu wako, apate kukubarikia katika nchi uingiayo kuimiliki.
Kumbukumbu la Sheria 30:15-16 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya; kwa hivi nikuagizavyo leo kumpenda BWANA, Mungu wako, kuenenda katika njia zake, na kushika maagizo yake, na amri zake, na hukumu zake, upate kuwa hai na kuongezeka; BWANA, Mungu wako, apate kukubarikia katika nchi uingiayo kuimiliki.
Kumbukumbu la Sheria 30:15-16 Neno: Bibilia Takatifu (NEN)
Tazama, naweka mbele yako leo uzima na mafanikio, mauti na maangamizo. Ninakuamuru leo kwamba umpende BWANA Mungu wako, utembee katika njia zake, na kutunza maagizo yake, amri na sheria zake; ndipo utakapoishi na kuongezeka, naye BWANA Mungu wako atakubariki katika nchi unayoingia kuimiliki.