Matendo 27:26-27
Matendo 27:26-27 Biblia Habari Njema (BHN)
Lakini ni lazima tutatupwa ufukoni mwa kisiwa fulani.” Usiku wa siku ya kumi na nne, tulikuwa tunakokotwa huku na huko katika bahari ya Adria. Karibu na usiku wa manane wanamaji walijihisi kuwa karibu na nchi kavu.
Matendo 27:26-27 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Lakini hatuna budi kupwelewa katika kisiwa kimoja. Hata usiku wa kumi na nne ulipofika, tulipokuwa tukichukuliwa huku na huko katika bahari ya Adria, kama usiku wa manane baharia wakadhani ya kuwa wanaikaribia nchi kavu.
Matendo 27:26-27 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Lakini hatuna budi kupwelewa katika kisiwa kimoja. Hata usiku wa kumi na nne ulipofika, tulipokuwa tukichukuliwa huko na huko katika bahari ya Adria, kama usiku wa manane baharia wakadhani ya kuwa wanaikaribia nchi kavu.
Matendo 27:26-27 Neno: Bibilia Takatifu (NEN)
Lakini hata hivyo meli yetu itakwama kwenye kisiwa fulani.” Usiku wa kumi na nne ulipofika, tulikuwa bado tunasukumwa na upepo katika Bahari ya Adria. Ilipokuwa yapata usiku wa manane, mabaharia wakahisi kwamba walikuwa wanakaribia nchi kavu.