Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 82

82
Ombi la kupata haki
Zaburi ya Asafu.
1 # Mhu 5:8; Kut 21:6 Mungu asimama katika kusanyiko la Mungu;
Katikati ya miungu anahukumu.
2 # Kum 1:17; Zab 58:1,2 Hadi lini mtahukumu kwa dhuluma,
Na kuzikubali nyuso za wabaya?
3Mfanyieni hukumu maskini na yatima;
Mtendeeni haki aliyeonewa, na fukara;
4Mwokoeni maskini na mhitaji;
Mwopoeni mikononi mwa wadhalimu.
5 # Zab 11:3 Hawajui wala hawafahamu, hutembea gizani;
Misingi yote ya nchi imetikisika.
6 # Ayu 21:32; Eze 31:14; Yn 10:34 Mimi nimesema, Ndinyi miungu,
Na wana wa Aliye Juu, enyi nyote.
7Lakini mtakufa kama wanadamu,
Mtaanguka kama mmoja wa wakuu.
8 # Zab 2:8; Ufu 11:15 Ee Mungu, usimame, uihukumu nchi,
Maana mataifa yote ni yako.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 82: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha