Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Wafilipi 3

3
1 # Flp 2:18; 4:4 Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana.
Kuondokana na yaliyopita
Kuwaandikieni mambo yale yale hakuniudhi mimi, bali kutawafaa ninyi.
2 # Ufu 22:15 Jihadharini na mbwa, jihadharini na watendao mabaya, jihadharini na wajikatao. 3#Rum 2:29 Maana sisi tu tohara, tumwabuduo Mungu kwa Roho, na kuona fahari juu ya Kristo Yesu, wala hatuutumainii mwili. 4#2 Kor 11:18,22 Lakini mimi ningeweza kuutumainia mwili. Mtu yeyote akijiona kuwa anayo sababu ya kuutumainia mwili, mimi zaidi. 5#Mdo 23:6; 26:5; Rum 11:1; Lk 1:59; 2:21 Nilitahiriwa siku ya nane, ni mtu wa taifa la Israeli, wa kabila la Benyamini, Mwebrania wa Waebrania, kwa habari ya kuishika torati, ni Farisayo, 6#Mdo 8:3; 22:4; 26:9-11 kwa habari ya juhudi, mwenye kuliudhi kanisa, kwa habari ya haki ipatikanayo kwa sheria sikuwa na hatia. 7#Mt 13:44,46 Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, niliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo. 8Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo; 9#Rum 3:21,22 tena nionekane katika yeye, nisiwe na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani iliyo katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu, kwa imani; 10#Rum 6:3-5; 8:17; Gal 6:17 ili nimjue yeye, na uweza wa kufufuka kwake, na ushirika wa mateso yake, nikifananishwa na kufa kwake; 11#Mdo 4:2; Ufu 20:5,6 ili nipate kwa njia yoyote kuufikia ufufuo wa wafu.
Kujitahidi kuelekea kwenye lengo
12 # 1 Tim 6:12; Mdo 9:6 Si kwamba nimekwisha kufika, au nimekwisha kuwa mkamilifu; la! Bali nakaza mwendo ili nipate kulishika lile ambalo kwa ajili yake nimeshikwa na Kristo Yesu. 13Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele; 14#1 Kor 9:24 nakaza mwendo, niifikie tuzo la thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu. 15#1 Kor 2:6 Basi sisi tulio wakamilifu na tuwaze hayo; na hata mkiwaza mengine katika jambo lolote, Mungu atawafunulia hilo nalo. 16#Gal 6:16 Lakini, hapo tulipofika na tuende katika lilo hilo.
17 # 1 Kor 4:16; 11:1; 1 The 1:7; 1 Pet 5:3 Ndugu zangu, mnifuate mimi, mkawatazame wao waendao kwa kuufuata mfano tuliowapa ninyi. 18#1 Kor 1:23; Gal 6:12 Maana wengi huenda, ambao nimewaambieni mara nyingi habari zao, na sasa nawaambia hata kwa machozi, kuwa ni adui za msalaba wa Kristo; 19#Rum 16:18 mwisho wao ni uharibifu, mungu wao ni tumbo, utukufu wao uko katika fedheha yao, waniao mambo ya duniani. 20#Efe 2:6; Kol 3:1; Ebr 12:22 Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo; 21#1 Kor 15:43,49,53 atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo aweza hata kuvitiisha vitu vyote viwe chini yake.

Iliyochaguliwa sasa

Wafilipi 3: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha