YouVersion Logo
Search Icon

Yona 2

2
Sala ya Yona
1Basi, Yona, akiwa tumboni mwa samaki huyo, akawa akimwomba Mwenyezi-Mungu, Mungu wake, 2akisema:
“Kwa sababu ya taabu yangu,
nilikuomba, ee Mwenyezi-Mungu,
nawe ukanisikiliza;
toka chini kuzimu, nilikulilia,
nawe ukasikiliza kilio changu.
3Ulinitupa katika kilindi, katikati ya bahari,
gharika ikanizunguka,
mawimbi na gharika vikapita juu yangu.
4Nilidhani kwamba nimetengwa nisiwe mbele yako;
nisiweze kuliona tena hekalu lako takatifu.
5Maji yalinizunguka na kunisonga;
kilindi kilinifikia kila upande,
majani ya baharini yakanifunika kichwa.
6Niliteremka hadi kwenye misingi ya milima,
katika nchi ambayo milango yake imefungwa milele.
Lakini wewe, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu,
umenipandisha hai kutoka humo shimoni.
7Roho yangu ilipoanza kunitoka,
nilikukumbuka, ee Mwenyezi-Mungu,
sala yangu ikakufikia,
katika hekalu lako takatifu.
8Watu wanaoabudu sanamu za miungu batili,
huutupilia mbali uaminifu wao kwako.
9Lakini mimi, kwa wimbo wa shukrani,
nitakutolea sadaka,
na kutimiza nadhiri zangu.
Mwenyezi-Mungu, ndiye aokoaye.”
10Basi, Mwenyezi-Mungu akamwamuru yule samaki, naye akamtapika Yona kwenye nchi kavu.

Currently Selected:

Yona 2: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy