Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Amani Ya KristoMfano

Amani Ya Kristo

SIKU 1 YA 3

Ninahubiri mara mbili kila Jumapili. Ibada ya kawaida katika kanisa ambapo mimi ni mchungaji huendeshwa kwa saa mbili, huku nusu ya muda huo ikitolewa kwa kuhubiri. Hiyo ina maana mimi huhubiri jumbe mbili za saa moja kila wiki. Pia mimi huwa na mikutano mifupi na viongozi wa kanisa kabla au baada ya kanisa. Zaidi ya hayo, ninafurahia chakula cha katikati ya asubuhi na mke wangu, watoto wetu na wajukuu.

Bila kusema, kufikia Jumapili alasiri, nimechoka. Hapo ndipo naelekea moja kwa moja kwenye kiti ninachokipenda kupumzika. Lakini kabla sijajua, huwa nimelala. Hakuna kitanda kinachohitajika. Hakuna blanketi inahitajika. Mto hauhitajiki. Ikiwa mpira wa miguu unaendelea, mimi hulala kabla ya mchezo na kukosa robo moja au mbili. Kila wiki nadhani hii itakuwa wiki ambayo nitakuwa mwanamume wa kutosha "kupumzika" kwa muda, na sitalala. Lakini mimi kawaida kufanya hilo ilo.

Yesu hakuwa ameegemea kwenye kiti cha kupumzikia katika Marko 4. Hakuwa akisinzia kwa kitikisa kichwa mbele ya mchezo wa kandanda huku tumbo lake likiwa limejaa chakula cha mchana. Ilikuwa usiku. Kulikuwa na giza. Kulikuwa na upepo. Mashua ilikuwa ikiyumba kwa nguvu katikati ya dhoruba kali iliyotishia kuizamisha. Unawezaje kulala wakati huo? Ni kweli kwamba, Yesu alikuwa amechoka sana baada ya siku ndefu ya kufundisha na kuhubiri, lakini alifanya mengi zaidi ya kutikisa kichwa tu. Yesu alipoenda kulala kwenye mashua, alifanya hivyo makusudi.

Ninajuaje hili? Kifungu kinatuambia. Mstari wa 38 unasema “alikuwa amelala juu ya mto.” Yesu alikuwa ameshika mto na kusogea upande wa nyuma—nyuma ya mashua—ambapo angeweza kujinyoosha na kujistarehesha! Ukiwa umejinyoosha, umelala kwenye mto, basi ulikuwa na maana ya kwenda kulala. Ikiwa una mto uliowekwa chini ya kichwa chako, huko ni kukoroma kwa makusudi.

Kwa hiyo Yesu angewezaje kulala kwenye dhoruba kali kama hiyo, wakati ambapo hata wanafunzi wake walihofia maisha yao? Labda alitaka kuwajaribu kama wangeamini neno lake au hali ya hewa. Alitaka kuona kama wangeamini kile alichosema zaidi ya hali zilizowazunguka.

Yesu alikuwa tayari amewaambia watakachofanya. Alikuwa amesema, “Na tuvuke mpaka ng’ambo ya pili ya bahari.” Yesu aliweza kulala katikati ya dhoruba kwa sababu ya sentensi hiyo moja. Hakusema, “Twendeni katikati ya bahari kisha tuzame na kufa maji.” Badala yake, Yesu alisema, “Na tuvuke mpaka ng’ambo ya bahari.” Hakuna dhoruba ambayo ingebadilisha mpango wake.

Wanafunzi wa Yesu walifanya yale tunayofanya mara nyingi tunapoenda kanisani. Walifanya yale tunayofanya mara nyingi tunaposikiliza mahubiri au kushiriki katika funzo la Biblia kama hili. Mara nyingi tunasikia ujumbe bila kutia maana. Ikiwa wanafunzi wangesikia maana iliyokusudiwa ya kile ambacho Yesu alikuwa amesema, labda wangenyakua mito yao wenyewe. Badala yake, walikuwa wamesikia maneno lakini walikosa kusikia ahadi.

Unapojikuta kwenye shida, usisahau ahadi. Kumbuka kile Yesu alisema. Yuko hapo pamoja nawe. Nyakua mto na kumwamini Yeye atulize mawimbi.

siku 2

Kuhusu Mpango huu

Amani Ya Kristo

Tunaweza kutarajia siku mbaya. Siku hizo huja kwa wanaoishi katika dunia iliyoanguka na ubinadamu ulioanguka. Kwa kweli, amani ingekuwa bidhaa adimu ikiwa tungetegemea hali zetu kama chanzo pekee cha amani hiyo. Ila bado...

More

Tungependa kuwashukuru The Urban Alternative (Tony Evans) kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: https://tonyevans.org/

Mipangilio yanayo husiana

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha