Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Soma Biblia Kila Siku Juni 2021Mfano

Soma Biblia Kila Siku Juni 2021

SIKU 1 YA 30

Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo ya wanadamu (m.8). Walimu wa dini ya Kiyahudi (wanatheolojia) walikuwa wametunga sheria nyingi za ziada kwa kufafanua sheria za Musa, kama m.3-5 inavyoonyesha: Mafarisayo na Wayahudi wote wasiponawa mikono mpaka kiwiko, hawali, wakishika mapokeo ya wazee wao; tena wakitoka sokoni, wasipotawadha, hawali; na yako mambo mengine waliyopokea kuyashika, kama kuosha vikombe, na midumu, na vyombo vya shaba. Basi wale Mafarisayo na waandishi wakamwuliza, Mbona wanafunzi wako hawaendi kwa kuyafuata mapokeo ya wazee, bali hula chakula kwa mikono najisi? Mafafanuzi haya kwa Wayahudi yalihesabika kuwa Neno la Mungu sawasawa na sheria ya Musa. Lakini jambo hili Yesu alilikanusha. Maana utakatifu wao ukiwa tofauti na mkazo wa amri ya Mungu, iliwafanya kuwa wanafiki, wakapotoka. Kwa hiyo Yesu akawaambia, Isaya alitabiri vema juu yenu ninyi wanafiki, kama ilivyoandikwa, Watu hawa huniheshimu kwa midomo Ila mioyo yao iko mbali nami; Nao waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu, Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo ya wanadamu (m.6-8). Je, wanatheolojia wa leo wakifundisha kinyume cha Neno la Mungu tutawafuata?

Andiko

siku 2

Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku Juni 2021

Soma Biblia Kila Siku Juni 2021 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia kila siku sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Marko na Ezekieli. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Karibu ku...

More

Tungependa kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha