Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Maelezo ya mpango

Somabiblia Kila Siku 3Mfano

Somabiblia Kila Siku 3

SIKU 2 YA 31

Yesu alipoiona huzuni ya Mariamu na wale waliokuja kumfariji akaugua rohoni mwake akalia machozi (m.33-36)! Akamwomba Baba yake amfufue Lazaro (m.41-42). Akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje. Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi ... (m.43-44). Ajabu sana, sivyo? Aliyetenda haya ni NENO ambaye kwa yeye vitu vyote vilifanyika: Hapo mwanzo kulikuwako Nneo, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika(Yn 1:1-3)! Kwa ishara hii Yesu alitukuzwa. Inathibitisha pia ukweli wa maneno yake aliyosema: Mimi ndimi ufufuo na uzima!

siku 1siku 3

Kuhusu Mpango huu

Somabiblia Kila Siku 3

SomaBiblia Kila Siku 3 ni mpango mzuri wa kukusaidia kusoma Biblia kwa njia rahisi. Ufafanuzi wa somo la kila siku unakupa mwanga na kiu ya kuendelea kulitafakari Neno la Mungu ukiwa peke yako au pamoja na wenzako.

Tungependa kushukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha