Kutoka 35:1-3
Kutoka 35:1-3 Biblia Habari Njema (BHN)
Mose alikusanya jumuiya yote ya Waisraeli, akawaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Mwenyezi-Mungu amewaamuru muyafanye: Kwa siku sita mtafanya kazi zenu; lakini siku ya saba ni Sabato siku ya mapumziko ambayo ni wakfu kwa Mwenyezi-Mungu. Yeyote atakayefanya kazi siku hiyo lazima auawe. Msiwashe hata moto katika makao yenu siku ya Sabato.”
Kutoka 35:1-3 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Musa akakutanisha mkutano wote wa wana wa Israeli, na kuwaambia, Maneno aliyoyausia BWANA ni haya, kwamba myafanye. Fanyeni kazi siku sita, lakini siku ya saba itakuwa siku takatifu kwenu; ni Sabato ya kustarehe kabisa kwa BWANA; mtu yeyote atakayefanya kazi yoyote katika siku hiyo atauawa. Hamtawasha moto katika nyumba zenu kwa siku ya Sabato.
Kutoka 35:1-3 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Musa akakutanisha mkutano wote wa wana wa Israeli, na kuwaambia, Maneno aliyoyausia BWANA ni haya, kwamba myafanye. Fanyeni kazi siku sita, lakini siku ya saba itakuwa siku takatifu kwenu; ni Sabato ya kustarehe kabisa kwa BWANA; mtu awaye yote atakayefanya kazi yo yote katika siku hiyo atauawa. Hamtawasha moto katika nyumba zenu kwa siku ya Sabato.
Kutoka 35:1-3 Neno: Bibilia Takatifu (NEN)
Mose akakusanya jumuiya yote ya Waisraeli na kuwaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo BWANA amewaamuru ninyi mfanye: Kwa siku sita, mtafanya kazi, lakini siku ya saba itakuwa takatifu kwenu, Sabato ya kupumzika kwa BWANA. Yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo ni lazima auawe. Msiwashe moto mahali popote katika makazi yenu siku ya Sabato.”