Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 82

82
Mungu mtawala mkuu
(Zaburi ya Asafu)
1Mungu anasimamia baraza lake;
anatoa hukumu katika kusanyiko la miungu:
2“Mpaka lini mtaendelea kuhukumu bila haki
na kuwapendelea watu waovu?
3Wapeni wanyonge na yatima haki zao;
tekelezeni haki za wanaoonewa na fukara.
4Waokoeni wanyonge na maskini,
waokoeni makuchani mwa wadhalimu.
5“Lakini nyinyi hamjui wala hamfahamu!
Nyinyi mnatembea katika giza la upotovu!
Misingi yote ya haki duniani imetikiswa!
6Mimi nilisema kuwa nyinyi ni miungu;
kwamba nyote ni watoto wa Mungu Mkuu!
7Hata hivyo, mtakufa kama watu wote;
mtaanguka kama mkuu yeyote.”
8Inuka ee Mungu, uuhukumu ulimwengu;
maana mataifa yote ni mali yako.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 82: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha