Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 128

128
Tuzo kwa jamaa imchayo Mungu
(Wimbo wa Kwenda Juu)
1Heri wote wamchao Mwenyezi-Mungu,
wanaoishi kufuatana na amri zake.
2Utapata matunda ya jasho lako,
utafurahi na kupata fanaka.
3Mkeo atakuwa kama mzabibu wa matunda mengi nyumbani mwako;
watoto wako kama chipukizi za mzeituni kuzunguka meza yako.
4Naam, ndivyo atakavyobarikiwa
mtu amchaye Mwenyezi-Mungu.
5Mwenyezi-Mungu akubariki kutoka Siyoni!
Uione fanaka ya Yerusalemu, siku zote za maisha yako.
6Uishi na hata uwaone wajukuu zako!
Amani iwe na Israeli!

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 128: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha