Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Isaya 12

12
Wimbo wa shukrani
1Siku hiyo mtasema:
“Nakushukuru, ee Mwenyezi-Mungu,
maana ingawa ulinikasirikia,
hasira yako imetulia,
nawe umenifariji.
2 #12:2 Taz Kut 15:2; Zab 118:14 Mungu ndiye mwenye kuniokoa,
nitamtegemea yeye, wala sitaogopa;
Mwenyezi-Mungu hunijalia nguvu;
yeye mwenyewe ndiye aniokoaye.”
3Mtachota maji kwa furaha
kutoka visima vya wokovu.
4Siku hiyo mtasema:
“Mshukuruni Mwenyezi-Mungu
mwombeni kwa jina lake.
Yajulisheni mataifa matendo yake,
tangazeni kuwa jina lake limetukuka.
5Mwimbieni Mwenyezi-Mungu sifa
kwa kuwa ametenda mambo makuu;
haya na yajulikane duniani kote.
6Pazeni sauti na kuimba kwa furaha,
enyi wakazi wa Siyoni,
maana aliye mkuu miongoni mwenu
ndiye Mungu, Mtakatifu wa Israeli.”

Iliyochaguliwa sasa

Isaya 12: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha