Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 99

99
Sifa kwa utukufu wa Mungu
1 # Kut 25:22 BWANA ametamalaki, mataifa wanatetemeka;
Ameketi juu ya makerubi, nchi inatikisika.
2BWANA ni mkuu katika Sayuni,
Naye ametukuka juu ya mataifa yote.
3 # Kum 28:58; Isa 6:3; Ufu 4:8 Na walisifu jina lake kuu litishalo;
Ndiye mtakatifu.
4 # Kum 32:3,4; Ayu 36:5; Isa 11:3-5; Yer 23:5; Mwa 18:25 Mfalme mkuu#99:4 Katika Kiebrania ni nguvu za mfalme. upendaye hukumu kwa haki;
Umeiimarisha haki;
Umefanya hukumu na haki katika Israeli.
5 # 1 Nya 28:2; Zab 132:7; Isa 66:1 Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;
Sujuduni penye kiti cha miguu yake;
Ndiye mtakatifu.
6Musa na Haruni walikuwa makuhani wake,
Na Samweli pia ni miongoni mwa walioliitia jina lake,
Walimlilia BWANA naye akawaitikia;
7 # Kut 19:9; 33:9; Hes 12:5 Akasema nao katika nguzo ya wingu.
Wakashika shuhuda zake na amri aliyowapa.
8 # Hes 14:20; Sef 3:7; Kum 9:20 Ee BWANA, Mungu wetu, ndiwe uliyewajibu;
Ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe
Ingawa uliwapatiliza matendo yao.
9Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;
Sujuduni mkiukabili mlima wake mtakatifu;
Maana BWANA, Mungu wetu, ni mtakatifu.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 99: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha