Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 91

91
Hakikisho la ulinzi wa Mungu
1Aketiye mahali pa siri pake Aliye Juu
Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.
2Atasema, BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu,
Mungu wangu nitakayemtumaini.
3Maana Yeye atakuokoa kutoka kwa mtego wa mwindaji,
Na katika maradhi mabaya.
4 # Zab 61:4 Kwa manyoya yake atakufunika,
Chini ya mbawa zake utapata kimbilio;
Uaminifu wake ni ngao na kigao.
5 # Ayu 5:19; Mit 3:23; Isa 43:2 Hutaogopa hatari za usiku,
Wala mshale urukao mchana,
6Wala mapigo yajayo usiku,
Wala maafa yatokeayo adhuhuri,
7Hata watu elfu wakianguka ubavuni pako.
Naam, watu elfu kumi katika mkono wako wa kulia!
Wewe hutakaribiwa na maafa.
8 # Mal 1:5 Ila kwa macho yako utatazama,
Na kuyaona malipo ya wasio haki.
9Kwa kuwa Wewe BWANA ndiwe kimbilio langu;
Umemfanya Aliye Juu kuwa makao yako.
10 # Mit 1:33; 2 The 3:3; 2 Pet 2:9 Mabaya hayatakupata wewe,
Wala tauni haitaikaribia hema yako.
11 # Mt 4:6; Lk 4:10 Kwa kuwa atakuagizia malaika wake
Wakulinde katika njia zako zote.#Zab 34:7; Mt 4:6; Lk 4:10; Ebr 1:14
12 # Ayu 5:23; Zab 37:24; Mt 4:6; Lk 4:11 Mikononi mwao watakuchukua,
Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
13 # Lk 10:19 Utawakanyaga simba na nyoka,
Mwanasimba na joka utawakanyaga kwa miguu.
14Kwa kuwa amekaza kunipenda
Nitamwokoa; na kumweka palipo juu,
Kwa kuwa amenijua Jina langu.
15 # Ayu 22:27; Zab 18:3; Yer 33:3; Zek 13:9; Ebr 5:7; Zab 43:2; 1 Sam 2:30 Ataniita nami nitamwitikia;
Nitakuwa pamoja naye taabuni,
Nitamwokoa na kumtukuza;
16Kwa siku nyingi nitamshibisha,
Nami nitamwonesha wokovu wangu.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 91: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha