Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 128:1-6

Zaburi 128:1-6 SRUV

Heri kila mtu amchaye BWANA, Aendaye katika njia yake. Taabu ya mikono yako hakika utaila; Utakuwa heri, na kwako kwema. Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao, Katika nyumba yako. Wanao watakuwa kama miche ya mizeituni Wakiizunguka meza yako. Tazama, atabarikiwa hivyo, yule amchaye BWANA. BWANA akubariki toka Sayuni; Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako; Naam, ukawaone wana wa wanao. Amani ikae na Israeli.

Soma Zaburi 128

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 128:1-6

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha