Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 120

120
Sala ya ukombozi
Wimbo wa Kupanda mlima.#120:1 Zaburi za 120-134 huenda ziliimbwa wakati wa kuhiji au kutoka kilimani Yerusalemu ambamo kulikuwa na lile hekalu.
1Katika shida yangu nilimlilia BWANA
Naye akaniitikia.
2Ee BWANA, uniponye
Na midomo ya uongo na ulimi wa hila.
3Akupe nini, akuzidishie nini,
Ewe ulimi wenye hila?
4Mishale ya mtu hodari iliyochongoka,
Pamoja na makaa ya mretemu.
5 # Mwa 10:2; 1 Sam 25:1; Yer 49:28 Ole wangu mimi!
Kwa kuwa ni mgeni katika Mesheki;
Na kufanya makao yangu
Katikati ya hema za Kedari.
6Kwa muda mrefu nimeishi,
Pamoja na watu wanaoichukia amani.
7Mimi nazingatia amani;
Bali ninenapo, wao wanataka vita.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 120: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha