Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Yona 2

2
Wimbo wa kushukuru
1Ndipo Yona akamwomba BWANA, Mungu wake, akiwa katika tumbo la yule samaki, 2Akasema,
Nilimlilia BWANA kwa sababu ya shida yangu,
Naye akaniitikia;
Katika tumbo la kuzimu niliomba,
Nawe ukasikia sauti yangu.
3 # Zab 88:6 Maana ulinitupa vilindini,
Ndani ya moyo wa bahari;
Gharika ya maji ikanizunguka pande zote;
Mawimbi yako yote na gharika zako zote zimepita juu yangu.
4 # Zab 31:22; Isa 49:14; 1 Fal 8:38 Nami nikasema, Nimetupwa mbali na macho yako;
Lakini nitatazama tena kukabili hekalu lako takatifu.
5Maji yalinizunguka, hata nafsini mwangu;
Vilindi vilinizunguka;
Mwani ulikizinga kichwa changu;
6Nilishuka hata pande za chini za milima;
Hiyo nchi ambayo mapingo yake yanafunga hata milele;
Lakini umeipandisha nafsi yangu kutoka humo shimoni,
Ee BWANA, Mungu wangu,
7 # Zab 18:6; 34:6; 130:2; Yer 2:13 Roho yangu ilipozimia ndani yangu,
Nilimkumbuka BWANA;
Maombi yangu yakakufikia,
Katika hekalu lako takatifu.
8 # 2 Fal 17:15; Zab 31:6; Yer 10:8 Watu waangaliao mambo ya ubatili na uongo
Hujitenga na rehema zao wenyewe.
9 # Zab 50:14; 66:13-15; Hos 14:2; Ebr 13:15 Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani;
Nitaziondoa nadhiri zangu.
Wokovu hutoka kwa BWANA.
10 # Yon 1:17; Mt 8:9 BWANA akasema na yule samaki, naye akamtapika Yona katika pwani.

Iliyochaguliwa sasa

Yona 2: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha