Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Waefeso 5

5
1 # Mt 5:48; Kol 3:12 Hivyo mwigeni Mungu, kama watoto wanaopendwa; 2#Kut 29:18; Zab 40:6; Gal 2:20; Ebr 10:10; Kol 3:13; Eze 20:41 mkaende katika upendo, kama Kristo naye alivyowapenda ninyi tena akajitoa kwa ajili yetu, sadaka na dhabihu kwa Mungu, kuwa harufu ya manukato.
Zikataeni njia za kipagani
3 # Efe 4:19; Kol 3:5 Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wowote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu; 4#Efe 4:29; Kol 3:8 wala aibu wala maneno ya upuzi wala ubishi; hayo hayapendezi; bali kuwepo kushukuru. 5#1 Kor 6:9,10; Kol 3:5; Mdo 8:21 Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, (ndiye mwabudu sanamu), aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu. 6#Rum 1:18; Kol 2:4,8 Mtu asiwadanganye kwa maneno yasiyo na maana; kwa kuwa kwa sababu ya hayo hasira ya Mungu huwajia wana wa uasi. 7Basi msishirikiane nao. 8#Efe 2:11,13; Lk 16:8; 1 Pet 2:9; Yn 12:36 Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, bali sasa mmekuwa nuru katika Bwana; nendeni kama watoto wa nuru, 9kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli; 10#Rum 12:2 mkihakiki ni nini impendezayo Bwana. 11#Yn 16:8 Wala msishirikiane na matendo yasiyozaa ya giza, bali myakemee; 12#Rum 1:24 kwa kuwa yanayotendeka kwao kwa siri, ni aibu hata kuyanena. 13#Yn 3:20,21 Lakini chochote kinachoangazwa na nuru hudhihirishwa, maana chochote kile kilichoadhihirika ni nuru. 14#Isa 26:19; 60:1; Rum 13:11; 6:13 Hivyo husema,
Amka, wewe usinziaye,
Ufufuke katika wafu,
Na Kristo atakuangaza.
15 # Mt 10:16; Kol 4:5 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; 16#Kol 4:5 mkiukomboa wakati kwa maana nyakati hizi ni za uovu. 17#Rum 12:2 Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana. 18#Mit 23:31; Lk 21:34 Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho; 19#Kol 3:16-17; Zab 33:2,3 mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu; 20#Kol 3:17 na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo.
Nyumba ya Kikristo
21 # 1 Pet 5:5 Hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo.
22 # Kol 3:18; 1 Pet 3:1; Mwa 3:16 Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. 23#1 Kor 11:3; Kol 1:18 Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. 24Lakini kama vile kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.
25 # Kol 3:19; 1 Pet 3:7 Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda kanisa, akajitoa kwa ajili yake; 26#Tit 3:5 ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; 27#Zab 45:13; 2 Kor 11:2 apate kujiletea kanisa tukufu, lisilo na dosari wala kunyanzi wala lolote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa. 28Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe. 29Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake popote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea kanisa. 30#Efe 1:23; 1 Kor 6:15; Mwa 2:23 Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. 31#Mwa 2:24 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. 32#Ufu 19:7 Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na kanisa. 33Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.

Iliyochaguliwa sasa

Waefeso 5: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha