Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

1 Mambo ya Nyakati 24

24
Mgawanyo wa makuhani
1 # Kut 6:23; Law 10:1; Hes 3:2; 26:60 Na zamu za wana wa Haruni ni hizi. Wana wa Haruni; Nadabu, na Abihu, na Eleazari, na Ithamari. 2#Hes 3:4; 26:61 Lakini hao Nadabu na Abihu walikufa kabla ya baba yao, wala hawakuwa na watoto; kwa hiyo Eleazari na Ithamari wakafanya ukuhani. 3Akawagawanya Daudi, na Sadoki wa wana wa Eleazari, na Ahimeleki wa wana wa Ithamari, katika utumishi kwa kadiri ya huduma yao. 4Wakaonekana wakuu wengi wa wana wa Eleazari kuliko wa wana wa Ithamari; wakagawanyika hivi; wa wana wa Eleazari kulikuwa na kumi na sita, waliokuwa wakuu wa koo za baba zao; na wa wana wa Ithamari, kulingana na koo za baba zao, wanane. 5#Yos 18:10; Mit 16:33; 18:18; Mdo 1:26 Ndivyo walivyogawanyika kwa kura, wao kwa wao; kwani kulikuwa na wakuu wa patakatifu, na watumishi wa Mungu, wa wana wa Eleazari, na wa wana wa Ithamari pia. 6#1 Fal 4:3; Neh 8:4 Naye Shemaya, mwana wa Nethaneli, mwandishi, aliyekuwa wa Walawi, akawaandika mbele ya mfalme, na mbele ya wakuu, na Sadoki kuhani, na Ahimeleki, mwana wa Abiathari, na wakuu wa koo za baba za makuhani, na za Walawi; ikatwaliwa ya Eleazari koo moja ya baba, na moja ikatwaliwa ya Ithamari. 7#Ezr 2:36; Neh 7:39 Kura ya kwanza ikamtokea Yehoiaribu, na ya pili Yedaya; 8#Ezr 10:21 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu; 9ya tano Malkia, ya sita Miyamini; 10#Neh 12:4,17; Lk 1:5 ya saba Hakosi, ya nane Abia; 11ya tisa Yeshua, ya kumi Shekania; 12ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu; 13ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu; 14ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri; 15ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi; 16ya kumi na tisa Pethahia, ya ishirini Ezekieli; 17ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli; 18ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia. 19#Hes 4:49; 1 Nya 9:25; 17:11-12; 2 Fal 5:7; Lk 1:8,23 Huu ndio utaratibu wa zamu zao katika huduma yao, ya kuingia nyumbani mwa BWANA kwa kadiri ya agizo lao, kwa mkono wa Haruni baba yao, kama BWANA, Mungu wa Israeli, alivyomwamuru.
Walawi wengineo
20 # 1 Nya 23:16 Na wa wana wa Lawi, waliosalia; wa wana wa Amramu, Shebueli; wa wana wa Shebueli, Yedeya. 21#1 Nya 23:17 Wa Rehabia; wa wana wa Rehabia, Ishia mkuu wao. 22#1 Nya 23:15 Wa Waishari, Shelomothi; wa wana wa Shelomothi, Yahathi. 23#1 Nya 15:9; 23:19 Na wana wa Hebroni; Yeria mkuu wao, Amaria wa pili, Yahazieli wa tatu, Yekameamu wa nne. 24Wana wa Uzieli, Mika; wa wana wa Mika, Shamiri. 25Nduguye Mika, Ishia; wa wana wa Ishia, Zekaria. 26#Kut 6:19; 1 Nya 23:21; Hes 3:20,33 Wana wa Merari; Mali na Mushi; wana wa Yaazia; Beno. 27Wana wa Merari; wa Yaazia; Beno, na Shohamu, na Zakuri, na Ibri. 28#1 Nya 23:22 Wa Mali; Eleazari, asiyekuwa na wana. 29Wa Kishi; wana wa Kishi; Yerameeli. 30#1 Nya 23:23 Na wana wa Mushi; Mali, na Ederi, na Yeremothi. Hao ndio wana wa Walawi, kwa kufuata koo za baba zao. 31Hao nao wakapigiwa kura vile vile, kama ndugu zao wana wa Haruni, machoni pa Daudi mfalme, na Sadoki, na Ahimeleki, na wakuu wa koo za baba za makuhani na za Walawi; koo za baba za mkuu, vile vile kama za nduguye mdogo.

Iliyochaguliwa sasa

1 Mambo ya Nyakati 24: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha