Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zab 76

76
Mungu wa Waisraeli - Mungu Mkuu
Kwa mwimbishaji: kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo.
1Katika Yuda Mungu amejulikana,
Katika Israeli jina lake ni kuu.
2Kibanda chake pia kiko Salemu,
Na maskani yake iko Sayuni.
3 # Zab 46:9; Eze 39:9 Huko ndiko alikoivunja mishale ya uta,
Ngao, na upanga, na zana za vita.
4 # Eze 38:12 Wewe U mwenye fahari na adhama,
Toka milima ya mateka.
5 # Isa 46:12; Zab 13:3; Yer 51:39 Wametekwa wenye moyo thabiti;
Wamelala usingizi;
Wala hawakuiona mikono yao
Watu wote walio hodari.
6 # Kut 15:1; Nah 2:13; Zek 12:4 Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo,
Gari na farasi wameshikwa na usingizi mzito.
7 # Ayu 41:10; Nah 1:6 Wewe ndiwe utishaye, naam, Wewe;
Naye ni nani awezaye kusimama ufanyapo hasira?
8Toka mbinguni ulitangaza hukumu;
Nchi iliogopa, ikakaa kimya.
9Mungu aliposimama ili kuhukumu
Na kuwaokoa wapole wa dunia wote pia.
10 # Kut 9:16 Maana hasira ya binadamu itakusifu,
Masalio ya hasira utajifunga kama mshipi.
11 # Mhu 5:4; Zab 68:29 Wekeni nadhiri, mkaziondoe
Kwa BWANA, Mungu wenu.
Wote wanaomzunguka wamletee hedaya,
Yeye astahiliye kuogopwa.
12 # Zab 68:35 Yeye huzikata roho za wakuu;
Na kuwatisha wafalme wa dunia.

Iliyochaguliwa sasa

Zab 76: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha