Siri ya BWANA iko kwao wamchao, Naye atawajulisha agano lake. Macho yangu humwelekea BWANA daima, Naye atanitoa miguu yangu katika wavu. Uniangalie na kunifadhili, Maana mimi ni mkiwa na mteswa. Katika shida za moyo wangu unifanyie nafasi, Na kunitoa katika dhiki zangu. Utazame teso langu na taabu yangu; Unisamehe dhambi zangu zote. Uwatazame adui zangu, maana ni wengi, Wananichukia kwa machukio ya ukali. Unilinde nafsi yangu na kuniponya, Nisiaibike, maana nakukimbilia Wewe. Ukamilifu na unyofu zinihifadhi, Maana nakungoja Wewe.
Soma Zab 25
Shirikisha
linganisha matoleo yote: Zab 25:14-21
Hifadhi mistari, soma bila mtandao, tazama klipu za mafunzo, na zaidi!
YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video