Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mdo 2

2
Kuja kwa Roho Mtakatifu
1 # Law 23:15-21; Kum 16:9-11; Mdo 1:14 Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. 2#Mdo 4:31Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. 3#Mt 3:11Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. 4#Mdo 4:31; 10:44-46; 19:6Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.
5 # Mdo 13:26 Na walikuwako Yerusalemu Wayahudi wakikaa, watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu. 6Basi sauti hii iliposikiwa makutano walikutanika, wakashikwa na fadhaa, kwa kuwa kila mmoja aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe. 7Wakashangaa wote, wakastaajabu wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya? 8Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa nayo? 9Warparthi na Wamedi na Waelami, nao wakaao Mesopotamia, Uyahudi na Kapadokia, Ponto na Asia, 10Frigia na Pamfilia, Misri na pande za Libia karibu na Kirene, na wageni watokao Rumi, Wayahudi na waongofu, 11Wakrete na Waarabu; tunawasikia hawa wakisema kwa lugha zetu matendo makuu ya Mungu. 12Wakashangaa wote wakaingiwa na shaka, wakiambiana, Maana yake nini mambo haya? 13Wengine walidhihaki, wakisema, wamelewa kwa mvinyo mpya.
Petro Ahutubia Mkutano
14Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu. 15Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana; 16#Yoe 2:28-32lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli,
17 # Yoe 2:28-32 Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto.
18Naam, na siku zile nitawamwagia watumishi wangu wanaume na wanawake Roho yangu, nao watatabiri.
19Nami nitatoa ajabu katika mbingu juu, na ishara katika nchi chini, damu na moto, na mvuke wa moshi.
20Jua litageuka kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla ya kuja ile siku ya Bwana iliyo kuu na iliyo dhahiri.
21 # Rum 10:13 Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa.
22 # Yn 3:2 Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua; 23#Mt 27:35; Mk 15:24; Lk 23:33; Yn 19:18; Mdo 4:28; 1 Pet 1:20mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua; 24#Mt 28:5-6; Mdo 3:15; Mk 16:6; Lk 24:5ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao. 25#Zab 16:8-11Maana Daudi ataja habari zake,
Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote,
Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.
26Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa,
ulimi wangu ukafurahi;
Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini.
27 # Mdo 13:35 Kwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu;
Wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifu.
28Umenijuvisha njia za uzima;
Utanijaza furaha kwa uso wako.
29 # Mdo 13:36; 1 Fal 2:10 Waume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo. 30#Zab 132:11; 89:3,4; 2 Sam 7:12-13Basi kwa kuwa ni nabii, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi; 31#Zab 16:10yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifu. 32Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake. 33#Mdo 1:4Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia. 34#Zab 110:1Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema,
Bwana alimwambia Bwana wangu,
Keti upande wa mkono wangu wa kuume.
35Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.
36 # Mdo 5:31 Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.
Waongofu wa Kwanza
37 # Mdo 16:30 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu? 38#Mdo 3:17-19; Lk 24:47Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. 39#Yoe 2:32; Isa 57:19Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie. 40#Kum 32:5; Flp 2:15Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi. 41#Mdo 4:4; 5:14Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu. 42#Mdo 20:7Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.
Maisha ya Waumini
43Kila mtu akaingiwa na hofu; ajabu nyingi na ishara zikafanywa na mitume. 44#Mdo 4:32-35Na wote walioamini walikuwa mahali pamoja, na kuwa na vitu vyote shirika, 45wakiuza mali zao, na vitu vyao walivyokuwa navyo, na kuwagawia watu wote kama kila mtu alivyokuwa na haja. 46#Mdo 2:42Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe, 47#Mdo 4:4; 5:14; 11:21; 14:1wakimsifu Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa.

Iliyochaguliwa sasa

Mdo 2: SUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha