Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 29

29
Zaburi 29
Sauti Ya Bwana Wakati Wa Dhoruba
Zaburi ya Daudi.
1 Mpeni Bwana, enyi mashujaa,
mpeni Bwana utukufu na nguvu.
2 Mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake;
mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
3 Sauti ya Bwana iko juu ya maji;
Mungu wa utukufu hupiga radi,
Bwana hupiga radi juu ya maji makuu.
4 Sauti ya Bwana ina nguvu;
sauti ya Bwana ni tukufu.
5 Sauti ya Bwana huvunja mierezi;
Bwana huvunja vipande vipande
mierezi ya Lebanoni.
6 Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama,
Sirioni#29:6 Yaani Mlima Hermoni. urukaruke kama mwana nyati.
7 Sauti ya Bwana hupiga kwa miali
ya umeme wa radi.
8 Sauti ya Bwana hutikisa jangwa;
Bwana hutikisa Jangwa la Kadeshi.
9 Sauti ya Bwana huzalisha ayala,
na huuacha msitu wazi.
Hekaluni mwake wote wasema,
“Utukufu!”
10 Bwana huketi akiwa ametawazwa juu ya gharika;
Bwana ametawazwa kuwa Mfalme milele.
11 Bwana huwapa watu wake nguvu;
Bwana huwabariki watu wake kwa kuwapa amani.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 29: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha