Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 129

129
Zaburi 129
Maombi Dhidi Ya Adui Za Israeli
Wimbo wa kwenda juu.
1 Wamenionea mno tangu ujana wangu;
Israeli na aseme sasa:
2 wamenionea mno tangu ujana wangu,
lakini bado hawajanishinda.
3 Wakulima wamelima mgongo wangu,
na kufanya mifereji yao mirefu.
4 Lakini Bwana ni mwenye haki;
amenifungua toka kamba za waovu.
5 Wale wote waichukiao Sayuni
na warudishwe nyuma kwa aibu.
6 Wawe kama majani juu ya paa,
ambayo hunyauka kabla hayajakua;
7 kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake,
wala akusanyaye kujaza mikono yake.
8 Wale wapitao karibu na wasiseme,
“Baraka ya Bwana iwe juu yako;
tunakubariki katika jina la Bwana.”

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 129: NEN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha