YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 99

99
Mungu mtawala mkuu
1Mwenyezi-Mungu anatawala,
mataifa yanatetemeka!
Ameketi juu ya viumbe vyenye mabawa,#99:1 viumbe vyenye mabawa: Taz. maelezo ya Mwa. 3:24
nayo dunia inatikisika!
2Mwenyezi-Mungu ni mkuu katika Siyoni;
ametukuka juu ya mataifa yote.
3Wote na walisifu jina lake kuu la kutisha.
Mtakatifu ndiye yeye!
4Ee mfalme mkuu, mpenda uadilifu!
Umethibitisha haki katika Israeli;
umeleta uadilifu na haki.
5Msifuni Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu;
angukeni kifudifudi mbele zake.
Mtakatifu ndiye yeye!
6Mose na Aroni walikuwa makuhani wake;
Samueli alikuwa miongoni mwa waliomlilia.
Walimlilia Mwenyezi-Mungu naye akawasikiliza.
7Alisema nao katika mnara wa wingu;
waliyazingatia matakwa yake na amri alizowapa.
8Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, wewe uliwasikiliza;
kwao ulikuwa Mungu mwenye kusamehe,
ingawa uliwaadhibu kwa makosa yao.
9Msifuni Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu;
abuduni katika mlima wake mtakatifu!#99:9 mlima wake mtakatifu: Taz Zab 2:6.
Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, ni mtakatifu.

Currently Selected:

Zaburi 99: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy