YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 97

97
Mungu mtawala mkuu
1Mwenyezi-Mungu anatawala!
Furahi, ee dunia!
Furahini enyi visiwa vingi!
2Mawingu na giza nene vyamzunguka;
uadilifu na haki ni msingi wa utawala wake.
3Moto watangulia mbele yake,
na kuwateketeza maadui zake pande zote.
4Umeme wake wauangaza ulimwengu;
dunia yauona na kutetemeka.
5Milima yayeyuka kama nta mbele ya Mwenyezi-Mungu;
naam, mbele ya Bwana wa dunia yote.
6Mbingu zatangaza uadilifu wake;
na mataifa yote yauona utukufu wake.
7Wote wanaoabudu sanamu wanaaibishwa,
naam, wote wanaojisifia miungu duni;
miungu yote husujudu mbele zake.
8Watu wa Siyoni wanafurahi;
watu wa Yuda wanashangilia,
kwa sababu ya hukumu zako, ee Mungu.
9Wewe Mwenyezi-Mungu ni mkuu juu ya dunia yote;
wewe watukuka juu ya miungu yote.
10Mwenyezi-Mungu huwapenda wanaochukia uovu,
huyalinda maisha ya watu wake;
huwaokoa makuchani mwa waovu.
11Mwanga humwangazia mtu mwadilifu,
na furaha kwa watu wanyofu wa moyo.
12Furahini kwa sababu ya Mwenyezi-Mungu enyi waadilifu;
mshukuruni kwa ajili ya jina lake takatifu.

Currently Selected:

Zaburi 97: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy