YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 90

90
KITABU CHA NNE
(Zaburi 90–106)
Mungu wa milele na binadamu kiumbe
(Sala ya Mose, mtu wa Mungu)
1Ee Bwana, tangu vizazi vyote,
wewe umekuwa usalama#90:1 neno kwa neno: Makao; hati nyingine: Kimbilio. wetu.
2Kabla ya kuwapo milima,
kabla hujauumba ulimwengu;
wewe ndiwe Mungu, milele na milele.
3Wamwambia binadamu, “Rudi mavumbini!”
Naye binadamu hurudi mavumbini alimotoka!
4 # Taz 2Pet 3:8 Kwako miaka elfu ni kama siku moja tu,
ni kama jana ambayo imekwisha pita;
kwako ni kama mkesha mmoja wa usiku!
5Wawafutilia mbali watu kama ndoto!
Binadamu ni kama nyasi zinazochipua asubuhi:
6Asubuhi huchipua na kuchanua,
jioni zimekwisha nyauka na kukauka.
7Hasira yako inatuangamiza;
tunatishwa na ghadhabu yako.
8Maovu yetu umeyaweka mbele yako;
dhambi zetu za siri ziko wazi mbele yako.
9Kwa hasira yako maisha yetu yatoweka,
yanaisha kama pumzi.
10Miaka ya kuishi ni sabini,
au tukiwa wenye afya, themanini;
lakini yote ni shida na taabu!
Siku zapita mbio, nasi twatoweka mara!
11Nani anayetambua uzito wa hasira yako?
Nani anayejali matokeo ya ghadhabu yako?
12Utufundishe ufupi wa maisha yetu
ili tuweze kuwa na hekima.
13Urudi, ee Mwenyezi-Mungu!
Utakasirika hata lini?
Utuonee huruma sisi watumishi wako.
14Utushibishe fadhili zako asubuhi,
tushangilie na kufurahi maisha yetu yote.
15Utujalie sasa miaka mingi ya furaha,
kama ulivyotupa miaka mingi ya shida na taabu.
16Utuoneshe matendo yako sisi watumishi wako;
uwaoneshe wazawa wetu uwezo wako mtukufu.
17Utufadhili ee Bwana, Mungu wetu;
uzitegemeze kazi zetu,
uzifanikishe shughuli zetu.

Currently Selected:

Zaburi 90: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy