YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 129

129
Sala dhidi ya maadui wa Israeli
(Wimbo wa Kwenda Juu)
1“Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu
Kila mtu katika Israeli na aseme:
2“Nimesumbuliwa vibaya tangu ujana wangu,
lakini hawakufaulu kunishinda.
3Walinijeruhi vibaya mgongoni mwangu,
wakafanya kama mkulima anayelima shamba.
4Lakini Mwenyezi-Mungu ni mwadilifu;
amezikata kamba za hao watu waovu.”
5Na waaibishwe na kurudishwa nyuma,
wote wale wanaouchukia mji wa Siyoni.
6Wawe kama nyasi juu ya paa la nyumba,
ambazo hunyauka kabla hazijakua,
7hakuna anayejishughulisha kuzikusanya,
wala kuzichukua kama matita.
8Hakuna apitaye karibu atakayewaambia:
“Mwenyezi-Mungu awabariki!
Twawabariki kwa jina la Mwenyezi-Mungu!”

Currently Selected:

Zaburi 129: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy