YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 111

111
Mungu asifika kwa matendo yake
1Msifuni Mwenyezi-Mungu!
Nitamshukuru Mwenyezi-Mungu kwa moyo wangu wote,
nikijumuika na jamii ya watu waadilifu.
2Matendo ya Mwenyezi-Mungu ni makuu mno!
Wote wanaoyafurahia huyatafakari.
3Kila afanyacho kimejaa utukufu na fahari;
uadilifu wake wadumu milele.
4Amesababisha matendo yake ya ajabu yakumbukwe;
Mwenyezi-Mungu ni mwema na mwenye huruma.
5Huwapa chakula wenye kumcha;
hasahau kamwe agano lake.
6Amewaonesha watu wake nguvu ya matendo yake,
amewapa nchi za mataifa mengine ziwe mali yao.
7Matendo yake ni ya haki na ya kuaminika;
kanuni zake zote ni za kutegemewa.
8Amri zake zadumu daima na milele;
zimetolewa kwa haki na uadilifu.
9Aliwakomboa watu wake
na kufanya nao agano la milele.
Yeye ni mtakatifu na wa kutisha mno!
10Kumcha Mwenyezi-Mungu ni msingi wa hekima;
wote wanaozitii amri zake hujaliwa busara.
Sifa zake zadumu milele.

Currently Selected:

Zaburi 111: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy