Kumcha Mwenyezi-Mungu ni msingi wa hekima; na kumjua yule Mtakatifu ni kupata akili. Kwa msaada wangu mimi Hekima siku zako zitaongezwa; utaongezewa miaka mingi maishani mwako. Kama una hekima, itakufaa wewe mwenyewe; kama ukiidharau, mwenyewe utapata hasara. Mwanamke mpumbavu ana kelele, hajui kitu wala hana haya. Hukaa kitako mlangoni mwa nyumba yake, huweka kiti chake mahali pa juu mjini, na kuwaita watu wapitao njiani, watu wanaokwenda kwenye shughuli zao: “Yeyote aliye mjinga na aje hapa!” Na yeyote aliye mpumbavu humwambia: “Maji ya wizi ni matamu sana; mkate unaoliwa kwa siri ni mzuri sana.” Lakini mjinga hajui kwamba humo mna wafu, wageni wa mwanamke huyo wamo chini Kuzimu.
Read Methali 9
Share
Compare All Versions: Methali 9:10-18
Save verses, read offline, watch teaching clips, and more!
YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy
Home
Bible
Plans
Videos