YouVersion Logo
Search Icon

Yobu 16

16
Jibu la Yobu
1Hapo Yobu akajibu:
2“Mambo kama hayo nimeyasikia mengi;
nyinyi ni wafariji duni kabisa!
3Mwisho wa maneno haya matupu ni lini?
Au ni kitu gani kinachowachochea kujibu?
4Kama nyinyi mngekuwa mimi, na mimi nyinyi,
ningeweza kusema kama nyinyi
ningeweza kubuni maneno dhidi yenu,
na kutikisa kichwa changu.
5Ningeweza kuwatia moyo kwa maneno yangu,
na maneno yangu ya faraja yangewatuliza.
6“Lakini nikisema maumivu yangu hayatulii,
na nikikaa kimya hayaondoki.
7Kweli Mungu amenichakaza#16:7-8 maana katika Kiebrania si dhahiri.
ameharibu kila kitu karibu nami.
8Amenifanya ninyauke, na huo ni ushindi dhidi yangu.
Kukonda kwangu kumenikabili
na kushuhudia dhidi yangu.
9Amenirarua kwa hasira na kunichukia;
amenisagia meno;
na adui yangu ananikodolea macho.
10Watu wananidhihaki na kunicheka;
makundi kwa makundi hunizunguka,
na kunipiga makofi mashavuni.
11Mungu amenitia mikononi mwa wajeuri,
na kunitupa mikononi mwa waovu.
12Nilikuwa nimestarehe, lakini akanivunjavunja,
alinikaba shingo na kunipasua vipandevipande;
alinifanya shabaha ya mishale yake,
13akanipiga mishale kutoka kila upande.
Amenipasua figo bila huruma,
na nyongo yangu akaimwaga chini.
14Hunivunja na kunipiga tena na tena;
hunishambulia kama askari.
15“Nimejishonea mavazi ya gunia,
fahari yangu nimeibwaga mavumbini.
16Uso wangu ni mwekundu kwa kulia,
kope zangu zimekuwa nyeusi ti;
17ingawa sijafanya dhuluma kwa mkono wangu,
na sala zangu kwa Mungu ni safi.
18“Ewe dunia, usiifunike damu yangu iliyomwagika;
kilio changu kienee kila mahali.
19 # Taz Yobu 19:25 Nina hakika ninaye shahidi wangu mbinguni,
mwenye kunitetea yuko huko juu.
20Rafiki zangu wanidharau;
nabubujika machozi kumwomba Mungu.
21Laiti mtu angenitetea mbele ya Mungu,
kama ifanyikavyo duniani kati za watu wawili.
22Naam, miaka yangu ni michache,
nami nitakwenda huko ambako sitarudi.

Currently Selected:

Yobu 16: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy