YouVersion Logo
Search Icon

Isaya 56

56
Wote wanakaribishwa
1Mwenyezi-Mungu asema:
“Zingatieni haki na kutenda mema,
maana nitawaokoeni hivi karibuni,
watu wataona wazi kwamba ninawakomboeni.
2Heri mtu anayezingatia kikamilifu ninayosema,
anayeshika sheria ya Sabato kwa heshima
na kuepa kutenda uovu wowote.
3“Mgeni anayenitambua mimi Mwenyezi-Mungu asifikiri:
‘Hakika Mwenyezi-Mungu atanitenga na watu wake.’
Naye towashi asiseme:
‘Mimi ni mti mkavu tu!’
4Maana mimi Mwenyezi-Mungu nasema:
Towashi ashikaye sheria zangu za Sabato,
anayefanya mambo yanayonipendeza,
na kulizingatia agano langu,
5nitampa nafasi maalumu na ya sifa
katika nyumba yangu na kuta zake;
nafasi bora kuliko kuwa na watoto wa kiume na wa kike:
Nitampa jina la kukumbukwa daima,
na ambalo halitafutwa kamwe.
6“Watu wageni watakaonikiri mimi Mwenyezi-Mungu,
watakaoniheshimu, wakapenda jina langu na kuwa watumishi wangu,
wote watakaoshika Sabato bila kuikufuru,
watu watakaozingatia agano langu,
7 #56:7 Taz Mat 21:13; Marko 11:17; Luka 19:46 hao nitawaleta katika mlima wangu mtakatifu,
na kuwafurahisha katika nyumba yangu ya sala;
tambiko na sadaka zao zitakubaliwa madhabahuni pangu.
Maana nyumba yangu itaitwa:
‘Nyumba ya sala kwa ajili ya watu wote’.
8“Hii ni kauli yangu mimi Bwana Mwenyezi-Mungu
ninayewakusanya Waisraeli waliotawanyika.
Licha ya hao niliokwisha kukusanya,
nitawakusanya watu wengine wajumuike nao.”
Viongozi wa Israeli walaumiwa
9Enyi wanyama wote wakali,
nanyi wanyama wote wa mwituni,
njoni muwatafune watu wangu.
10Maana viongozi wao wote ni vipofu;
wote hawana akili yoyote.
Wote ni kama mbwa bubu wasiobweka,
hulala tu na kuota ndoto,
hupenda sana kusinzia!
11Hao ni kama mbwa wenye uchu sana,
wala hawawezi kamwe kutoshelezwa.
Wachungaji hao hawana akili yoyote;
kila mmoja hutafuta faida yake mwenyewe.
12Huambiana, “Njoni, twende kutafuta divai;
njoni tunywe tushibe pombe!
Kesho itakuwa kama leo,
tena itakuwa sikukuu kubwa zaidi.”

Currently Selected:

Isaya 56: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy