YouVersion Logo
Search Icon

Zab 99

99
Sifa kwa Utukufu wa Mungu
1 # Kut 25:22 BWANA ametamalaki, mataifa wanatetemeka;
Ameketi juu ya makerubi, nchi inatikisika.
2BWANA katika Sayuni ni mkuu,
Naye ametukuka juu ya mataifa yote.
3 # Kum 28:58; Isa 6:3; Ufu 4:8 Na walishukuru jina lake kuu la kuhofiwa;
Ndiye mtakatifu.
4 # Kum 32:3,4; Ayu 36:5; Isa 11:3-5; Yer 23:5; Mwa 18:25 Nguvu za mfalme nazo zapenda hukumu;
Wewe ndiwe uliyeithibitisha adili;
Ulifanya hukumu na haki katika Yakobo.
5 # 1 Nya 28:2; Zab 132:7; Isa 66:1 Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;
Sujuduni penye kiti cha miguu yake;
Ndiye mtakatifu.
6Musa na Haruni miongoni mwa makuhani wake,
Na Samweli miongoni mwao waliitiao jina lake,
Walipomwita Bwana aliwaitikia;
7 # Kut 19:9; Kut 33:9; Hes 12:5 Katika nguzo ya wingu alikuwa akisema nao.
Walishika shuhuda zake na amri aliyowapa.
8 # Hes 14:20; Sef 3:7; Kum 9:20 Ee BWANA, Mungu wetu, ndiwe uliyewajibu;
Ulikuwa kwao Mungu mwenye kusamehe
Ingawa uliwapatiliza matendo yao.
9Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;
Sujuduni mkiukabili mlima wake mtakatifu;
Maana BWANA, Mungu wetu, ndiye mtakatifu.

Currently Selected:

Zab 99: SUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy