YouVersion Logo
Search Icon

Ezr 1

1
Wayahudi Waachiliwa kutoka Babeli
1 # 2 Nya 36:22; Yer 25:12; Law 26:42; Ezr 5:13 Ikawa katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, ili kwamba neno la BWANA alilolisema kwa kinywa cha Yeremia lipate kutimizwa, BWANA akamwamsha roho yake Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata akapiga mbiu katika ufalme wake wote, akaiandika pia, akisema,
2 # Isa 44:28 Koreshi, mfalme wa Uajemi asema hivi;
BWANA, Mungu wa mbinguni, amenipa falme zote za dunia; naye ameniagiza nimjengee nyumba katika Yerusalemu, ulioko Yuda. 3#Kum 3:24; 2 Sam 22:32; Zab 86:10; Isa 37:16; Dan 6:26; Mk 12:32; 1 Kor 8:6Basi kila mtu katika ninyi nyote mlio watu wake, BWANA, Mungu wake, na awe pamoja naye, na akwee mpaka Yerusalemu, ulioko Yuda, akaijenge nyumba ya BWANA, Mungu wa Israeli, (yeye ndiye Mungu), iliyoko Yerusalemu. 4Na mtu awaye yote aliyesalia mahali po pote akaapo hali ya ugeni, na asaidiwe na watu wa mahali pake, kwa fedha, na dhahabu, na mali, na wanyama, zaidi ya vitu vitolewavyo kwa hiari ya mtu, kwa ajili ya nyumba ya Mungu, iliyoko Yerusalemu.
5 # Mit 16:1; Flp 2:13 Ndipo wakaondoka wakuu wa mbari za mababa, wa Yuda na Benyamini, na makuhani, na Walawi, naam, watu wote ambao Mungu amewaamsha roho zao kukwea, ili kuijenga nyumba ya BWANA, iliyoko Yerusalemu. 6Na watu wote waliokaa karibu nao pande zote wakawatia nguvu mikono yao, kwa vyombo vya fedha, kwa dhahabu, kwa mali, na kwa wanyama, na vitu vya thamani, zaidi ya vile vilivyotolewa kwa hiari ya mtu. 7#Ezr 5:14; 6:5; 2 Fal 24:13; 2 Nya 36:7Tena Koreshi, mfalme, alivitoa vyombo vya nyumba ya BWANA, alivyokuwa amevileta Nebukadreza#1:7 Au, Nebukadneza. toka Yerusalemu, na kuvitia katika nyumba ya miungu yake. 8#Ezr 5:14; Hag 1:1Naam, vyombo vile ndivyo alivyovitoa Koreshi, mfalme wa Uajemi, kwa mkono wa Mithredathi, mtunza hazina; naye akavihesabu mbele ya Sheshbaza, mkuu wa Yuda. 9Na hii ndiyo hesabu yake; sinia za dhahabu thelathini, sinia za fedha elfu, visu#1:9 Au, vyetezo. ishirini na kenda; 10mabakuli ya dhahabu thelathini, mabakuli ya fedha ya namna ya pili mia nne na kumi,#1:10 Au; mabakuli ya fedha elfu mbili mia nne na kumi. na vyombo vingine elfu. 11Vyombo vyote vya dhahabu na vya fedha vilikuwa jumla yake elfu tano na mia nne. Hivyo vyote Sheshbaza akakwea navyo, hapo walipokwea wale wa uhamisho kutoka Babeli mpaka Yerusalemu.

Currently Selected:

Ezr 1: SUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy