YouVersion Logo
Search Icon

Efe 5

5
1 # Mt 5:48; Kol 3:12 Hivyo mfuateni Mungu, kama watoto wanaopendwa; 2#Kut 29:18; Zab 40:6; Gal 2:20; Ebr 10:10; Kol 3:13; Eze 20:41mkaenende katika upendo, kama Kristo naye alivyowapenda ninyi tena akajitoa kwa ajili yetu, sadaka na dhabihu kwa Mungu, kuwa harufu ya manukato.
Zikataeni Njia za Kipagani
3 # Efe 4:19; Kol 3:5 Lakini uasherati usitajwe kwenu kamwe, wala uchafu wo wote wa kutamani, kama iwastahilivyo watakatifu; 4#Efe 4:29; Kol 3:8wala aibu wala maneno ya upuzi wala ubishi; hayo hayapendezi; bali afadhali kushukuru. 5#1 Kor 6:9,10; Kol 3:5; Mdo 8:21Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu. 6#Rum 1:18; Kol 2:4,8Mtu asiwadanganye kwa maneno yasiyo na maana; kwa kuwa kwa sababu ya hayo hasira ya Mungu huwajia wana wa uasi. 7Basi msishirikiane nao. 8#Efe 2:11,13; Lk 16:8; 1 Pet 2:9; Yn 12:36Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, bali sasa mmekuwa nuru katika Bwana; enendeni kama watoto wa nuru, 9kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli; 10#Rum 12:2mkihakiki ni nini impendezayo Bwana. 11#Yn 16:8Wala msishirikiane na matendo yasiyozaa ya giza, bali myakemee; 12#Rum 1:24kwa kuwa yanayotendeka kwao kwa siri, ni aibu hata kuyanena. 13#Yn 3:20,21Lakini yote yaliyokemewa hudhihirishwa na nuru maana kila kilichodhihirika ni nuru. 14#Isa 26:19; 60:1; Rum 13:11; 6:13Hivyo husema,
Amka, wewe usinziaye,
Ufufuke katika wafu,
Na Kristo atakuangaza.
15 # Mt 10:16; Kol 4:5 Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; 16#Kol 4:5mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu. 17#Rum 12:2Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana. 18#Mit 23:31; Lk 21:34Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho; 19#Kol 3:16-17; Zab 33:2,3mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu; 20#Kol 3:17na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;
Nyumba ya Kikristo
21 # 1 Pet 5:5 hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo.
22 # Kol 3:18; 1 Pet 3:1; Mwa 3:16 Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii Bwana wetu. 23#1 Kor 11:3; Kol 1:18Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. 24Lakini kama vile Kanisa limtiivyo Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.
25 # Kol 3:19; 1 Pet 3:7 Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; 26#Tit 3:5ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; 27#Zab 45:13; 2 Kor 11:2apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa. 28Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe. 29Maana hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa. 30#Efe 1:23; 1 Kor 6:15; Mwa 2:23Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. 31#Mwa 2:24Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. 32#Ufu 19:7Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa. 33Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe.

Currently Selected:

Efe 5: SUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy